• About Us!
  • Contact us
  • Home 1
  • Privacy Policy
Sunday, March 19, 2023
  • Login
  • Home
  • TVET COLLEGE
  • Academic calendar
  • Australia University
  • Manager login
  • TargetPayandBenefits
No Result
View All Result
24infoz.com
  • Home
  • TVET COLLEGE
  • Academic calendar
  • Australia University
  • Manager login
  • TargetPayandBenefits
No Result
View All Result
24infoz.com
No Result
View All Result
Home MUSIC

Matola: Naondoka Simba

thiszmenasog by thiszmenasog
March 16, 2023
in MUSIC, Uncategorized
0 0
0
Matola: Naondoka Simba
Share on FacebookShare on Twitter

By Thobias Sebastian

Mwananchi Communications Limited (MCL)

KOCHA Msaidizi wa Simba, Seleman Matola amelithibitishia Mwanaspoti kwamba anaondoka kwenye benchi la ufundi la timu hiyo kwa muda akapige shule kidogo.

Matola ambaye ni nahodha wa zamani wa Simba na Taifa Stars, amepata fursa ya kwenda kusoma kozi ya leseni A ya CAF, ataanza Novemba 21 ambapo atasoma kwa wiki mbili, kisha atarejea kikosini hapo kwa kuyafanyia kazi kwa vitendo mafunzo aliyoyapata. Hiyo inamaanisha kwamba Matola hatokuwepo mpaka mwanzoni mwa mwezi Desemba.

Matola ambaye aliwahi kucheza Supersport ya Afrika Kusini amesema; “Nisingeweza kukataa fursa hiyo, lakini sitaacha kuitakia mema timu yangu, nitakuwa nawasiliana na kocha, kuhakikisha tunashauriana ili Simba ibaki kuwa imara kwa muda wote inapocheza ligi ya ndani na Ligi ya Mabingwa Afrika.

“Nilishaongea na viongozi kila kitu kuhusu kozi hii, naamini watakuwa wanalifanyia kazi suala hilo, Simba ni klabu kubwa itaweka sawa kila kitu, zaidi ya hayo yote namshukuru Mungu kupata fursa hiyo na uzuri nitakuwa narejea kwenye klabu yangu kufanya mafunzo ya vitendo.”

Simba kwa kipindi hiki haina kocha wa makipa, baada ya Mwarami Mohamed kutokuwepo kikosini kuanzia mechi yao iliyopita dhidi ya Singida Big Stars ikitoka kwa sare ya bao 1-1, ikielezwa ana ‘matatizo ya kifamilia’.

Matola ambaye ana leseni B ya ukocha anakwenda kusoma kozi nyingine ya leseni A ya CAF nje ya Jiji Dar es Salaam ambapo atashindwa kufanya majukumu mawili kwa wakati mmoja.

Mabosi wa Simba watalazimika sasa kuboresha benchi la ufundi kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma kocha huyo alipokwenda kusoma timu ikiwa chini ya Didier Gomes ambapo alitafutiwa msaidizi wake Thierry Hitimana na baadaye Matola aliungana nao alipomaliza masomo yake.

Habari za ndani kutoka Simba pia zinaeleza kwamba kipa wao wa zamani Juma Kaseja huenda akala shavu kwa kipindi hiki ingawa bado linaendelea kujadiliwa suala lake. Kaseja kwasasa ni kocha wa makipa wa Taifa Stars na timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 23 ‘Ngorongoro Heroes’.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa upande wa kocha wa viungo ambaye nafasi yake ilikuwa wazi kwa muda mrefu tayari amepatikana ingawa hajatangazwa ingawa Mwanaspoti linafahamu kwamba anaweza akatangazwa muda wowote kuanzia sasa.

Kwa mara ya mwisho Simba ilikuwa na mtaalamu wa viungo Sbai Karim kutoka Tunisia aliondolewa pamoja na kocha Maki Zoran na kocha wa makipa alikuwa Mohamed Rachid raia wa Morocco.

Endapo uongozi wa klabu hiyo hautachukua hatua za haraka, watampa kazi ngumu Juma Mgunda kusimamia benchi hilo katika mechi dhidi ya Mbeya City (Novemba 23), Polisi Tanzania (Novemba 27), Coastal Union (Desemba 3), wakati mechi inayofuata dhidi ya Geita Gold itakuwa ni Desemba 18.

Hata hivyo, mabosi wa Simba walipotafutwa ili kuelezea hali hiyo ya benchi la ufundi simu zao za mkononi hazikupokelewa huku ikielezwa kuwa walikuwa kwenye kikao kizito cha ndani.

Simba imepania kufanya vizuri msimu huu hususani kimataifa ambako lengo ni kwenda nusufainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

thiszmenasog

thiszmenasog

Next Post
ZA NDAANI KABISA: Yanga bado inampigia hesabu Mbrazil

ZA NDAANI KABISA: Yanga bado inampigia hesabu Mbrazil

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Connect with us

  • 121 Followers
  • 23.8k Followers
  • Trending
  • Comments
  • Latest

Form one selection 2023 Tanzania

December 16, 2022
Form Four results 2022

Form Four results 2022

January 20, 2023
The 2023 Matric results

The 2023 Matric results

January 20, 2023
Management and Development for Health (MDH)

16 New Job Vacancies at Management and Development for Health (MDH)

February 11, 2023
login

Life science grade 12 practical investigation 2023 term 1

0
University of South Australia academic calendar 2023/2024

Swinburne University of Technology academic calendar 2023/2024

0
University of South Australia academic calendar 2023/2024

University of Southern Queensland academic calendar 2023/2024 – USQ academic calendar 2023-2024

0
University of South Australia academic calendar 2023/2024

Kaplan Business School academic calendar 2023/2024 – kaplan study periods 2023

0
login

Life science grade 12 practical investigation 2023 term 1

February 21, 2023
Paycom

Best brain mock questions 2023 for jhs 3 download

February 21, 2023
Management and Development for Health (MDH)

16 New Job Vacancies at Management and Development for Health (MDH)

February 11, 2023
Northeastern university acceptance rate

Northeastern university acceptance rate

February 11, 2023

Recommended

login

Life science grade 12 practical investigation 2023 term 1

February 21, 2023
Paycom

Best brain mock questions 2023 for jhs 3 download

February 21, 2023
Management and Development for Health (MDH)

16 New Job Vacancies at Management and Development for Health (MDH)

February 11, 2023
Northeastern university acceptance rate

Northeastern university acceptance rate

February 11, 2023
  • Home
  • TVET COLLEGE
  • Academic calendar
  • Australia University
  • Manager login
  • TargetPayandBenefits

© 2023 24INFOS

No Result
View All Result
  • Home
  • TVET COLLEGE
  • Academic calendar
  • Australia University
  • Manager login
  • TargetPayandBenefits

© 2023 24INFOS

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Create New Account!

Fill the forms below to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In